Wokovu
ni mpango aliouandaa Mungu mwenyewe wa kumtafuta mwanadamu aliyepotea na
kumleta awe chini ya milki yake. Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote
imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi
kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;(Tito 2:11-12), maandiko yanatuambia ya kuwa neema hii
inatufundisha kukataa ubaya na tama za kidunia
au kwa maana nyingine hii neema imekuja ili tuache uovu au tuache dhambi na baada ya kuziicha
dhambi tuishi maisha ya kiasi, na haki, na utauwa (utakatifu). Biblia inaposema
hii neema ni kwa ajili ya wanadamu wote in maana ya kuwa haikutoka kwa mwanadamu
awaye yote bali ilitoka kwa Mungu mwenyewe na kwa kuwa inatoka kwa Mungu basi
ujue inamgusa kila mwanadamu na ndani yake imejaa mafundisho ya kutuelekeza ni
kwa namna gani tunaweza kuishi katika ulimwengu huu wa sasa na si ule ujao bali
ulimwengu huu wa sasa; na hapa ndipo tunapopata jibu kuwa kuokoka ni hapa
duniani na sio mbinguni.
Wokovu
sio dini kama wengine wanavyodhani, wala
sio dhehebu fulani wala ubatizo fulani bali wokovu ni mpango unaotoka kwa Mungu
mwenyewe na lazima uendane na kuacha na kuchukia uovu na kuamua kuishi maisha
mengine tofauti na ambayo ulikuwa unaishi awali na hayo maisha yawe
yanaratibiwa na Roho Mtakatifu kila siku.
Tunaposema
ni neema ya Mungu maana yake, Mungu huitoa bure pasipo malipo wala gharama
zozote bali yeye mwenyewe Mungu amekwisha kulipa gharama zote. (Free of cost)
NINI
MAANA YA KUOKOKA.
Kuna
maana mbalimbali au tafsiri nyingi juu ya kuokoka ila na tuangalie maana chache
katika maandiko jinsi yasemavyo.
Kuokoka
ni kuzaliwa mara ya pili. (Yohana 3:1-6), mstari wa 3 unasema hivi; Yesu
akajibu, akamwambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa
Mungu. Na mstari wa 6 wa Yohana 3 unasema; Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili;
na kilichozaliwa kwa Roho ni roho. Kinachofanyika baada ya mtu
kumkubali Kristo maishani mwake Roho Mtakatifu anamzaa tena huyu mtu kwa jinsi
ya roho haijalishi ni mtu mzima au mtoto; badiliko linatokea rohoni ambalo halionekani kwa jinsi ya mwili.
Ndani mwako unafanyika kiumbe kipya (2
Kor 5:17) utu wako wa kale ulionao unavuliwa na Roho Mtakatifu na unavikwa
utu upya na ndiyo maana maandiko yanasema ya kuwa unazaliwa kwa maraya pili.
Maana
nyingine ni; Kuamini na kukiri ya kuwa Yesu ni Bwana na kuishi kama ulinyokiri.
(Rum 10:9-10), Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini
moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo
mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kuokoka lazima kuendane na kukiri kwa kinywa na kuamini ndani ya moyo juu ya
Yesu Kristo na maisha yako yaendane kama ulivyokiri na kuamini, hili ni jambo
muhimu sana katiaka maisha ya mtu aliyeokoka , wapo walokole wengi sana leo
ambao wanamuaibisha Yesu kwa sababu wanaishi kinyume na walivyokiri na ni jambo
ambalo linamuhuzunisha Mungu sana. Kwa mfano; mtu anaweza kuwa ameokoka lakini
bado ni mzinzi, mwasherati, msengenyaji na nk. Mungu na atusaidie sana!! Amen.
TOFAUTI
KATI YA DINI NA WOKOVU
Dini
ni mpango wa mwanadamu wa kumtafuta na kumwabudu Mungu, inaweza kuwa ni Mungu
aliye hai (The Most High) au miungu. (gods), {Kutoka 32:1-8}…wamejifanyizia
ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu
yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri. Hii ina maana
mwanadamu akikosa cha kuabudu ataabudu chochote alichokichagua kuwa mungu wake.
Jambo
ambalo nataka ulielewe mpendwa katika Kristo ni kwamba hakuna hata dini moja
duniani ambayo inaweza kumfikisha mwanadamu mbinguni ila YESU peke yake ndiye
awezaye kufikisha mwanadamu kwenye uzima wa milele. Mungu anatuhitaji
kuuthamini wokovu maana Yesu alipokuja duniani alizikuta dini na aliziacha dini;
alichokihitaji Yesu hadi leo ni wote wenye mwili wamuamini yeye peke yake ili
aweze kuwaokoka na kuwapa uzima wa milele.
Wokovu
kama tulivyoona awali, ni mpango wa Mungu mwenyewe wa kumtafuta mwanadamu
aliyepotea (katika dhambi) na kumfanya awe chini ya milki/utawala au chini ya
utaratibu/mfumo wake. (Tito 2:11-12).
FAIDA ZA
KUOKOKA
Zipo
faida nyingi sana ambazo mtu aliyeokoka anatakiwa kuzipata wakati akiendelea
kumtukuza Mungu hapa duniani, hizi nilizokuandikia hapa ni chache kati ya
nyingi. Roho Mtakatifu ataendelea kukufundisha njia nyingine kadri
unavyoendelea kukua kiroho.
Tunasamehewa
dhambi zote.
Mdo
10:43 Isaya 44:22
Zab
103:12 Isaya 43:25
Tunafanyika
wana wa Mungu.
Yoh 1:12 Rum 8:15-16
Tunapata
uzima wa milele
1 Yoh 5:13 Yoh 20:31
Roho
Mtakatifu anakaa ndani yetu.
1 Kor 3:16-17 2 Kor 6:16
1 Kor 6:19-20 Rum 8:9-10
Tunavikwa
utu upya.
2 Kor 5:17 Efeso 4:22-24
Yesu
anafanya makao kwetu.
Ufunuo 3:20 Yoh 15:14-15
NITAJUAJE
KAMA NIMEOKOKA?
Inawezekana
umewahi kukutana na swali la namna hii au umewahi kusikia watu wakiulizwa swali
kama hili ya kwamba ni kitu gani kinachomfanya mtu ajue ya kuwa ameokoka je,
ingekuwa wewe leo unaulizwa swali la jinsi hii ungejibuje? Hebu tuangalie
maandiko yanasemaje.
(Rum
8:16), Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa
Mungu; hii ni sababu mojawapo inayotupa uhakika ndani yetu ya kuwa sisi
tumeokoka maana Roho Mtakatifu aliye ndani yetu anatushuhudia ya kuwa sisi tu
watoto wa Mungu, ambao ndani yetu hakuna tena hukumu y dhambi inayotushaki ya
kuwa sisi tu watenda dhambi wala hakuna hofu ya jehanamu kwa sababu watoto wa
Mungu kwao ni mbinguni na si jehanamu.
Sababu
ya pili tunaipata katika kitabu cha waraka wa kwanza wa Yohana, sura ya tano na
mstari wa kumi na tatu (1 Yohana 5:13), Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya
kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu.
Maandiko yanena wazi ya kuwa uzima wa milele unakaa ndani yetu sisi
tulioliamini jina la Yesu Kristo; uzima wa milele maana yake ni maisha ya
milele (eternal life) yapo kwa
waliookoka, Yesu ndiye atupaye huo uzima wa milele pamoja na Roho Mtakatifu
aliye ndani yetu. Haleluya!
JE,
NISIPOOKOKA NITAFIKA MBINGUNI?
Jibu
ni rahisi sana, hapana huwezi kufika mbinguni, kwa sababu:-
(Yohana
3:18), Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu
hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. Biblia inasema wazi hata kama
ungali hai leo lakini kama hujamwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa
maisha yako; umekwisha kuhukumiwa tayari hata kama siku ya hukumu haijafika, na
ikitokea ukifa leo kama bado hujamwamini Yesu Kristo huwezi kwenda mbinguni.
Yesu
akamwambia, mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa
njia ya mimi.
(Yoh 14:6), kuna mambo matatu hapa maandiko yanataja sifa au uwezo alionao
Yesu, anasema yeye ni njia, kweli, na uzima; hatuwezi kumfikia Mungu wala kumuona kwa namna yoyote ile
isipokuwa Yesu Kristo mwenyewe ametupa
kibali cha kufika mbele za Mungu. Amen! Amen!.
N
|
atumaini
ndugu mpendwa umepata msaada wa kukusaidia juu ya somo hili, ni maombi yangu
kwako Mungu azidi kuweka ndani yako roho ya kupenda kujifunza ili uzidi kukua
katika kumwishia yeye siku zote za maisha yako.
Usisite
kuniandikia au kunipigia simu pale ambapo utakuwa una maswali au una hitaji
tumuombe Mungu kwa pamoja katia jambo ambalo umekutana nalo na kwako limekupa
ni tatizo, maana sisi tu viungo vya Kristo tukitegemeana kila kimoja na
chenzake ili kwa pamoja tuweze kuujenga mwili wa Kristo.
Na
Mungu wangu akubariki sana unapokwenda kuyaweka kwenye matendo yale ambayo Roho
Mtakatifu amekufundisha katika somo hili, sifa na heshima ni za kwake kwa maana
anastahili.
Good Bless you for what you are doing!
ReplyDeleteAmen Amen..thanx for your concern
Deletebe blessed more
ReplyDeleteMungu akubariki nimeipenda tena imenifungua
ReplyDeleteMy God bless you my friend
ReplyDeleteGod bless you too.
ReplyDelete